Pata taarifa kuu

Senegal: Serikali inasema inachukua hatua kudumisha amani na utulivu

Nairobi – Wizara ya mambo ya ndani nchini Senegal, imesema inachukua hatua kuhakikisha kuna utulivu na amani kwenye taifa hilo haswa wakati huu maandamano ya upinzani yakiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya sehemu za taifa hilo.

Polisi nchini Senegal wamekuwa wakikabiliana na wafuasi wa Ousmane Sonko mjini Dakar na sehemu zengine
Polisi nchini Senegal wamekuwa wakikabiliana na wafuasi wa Ousmane Sonko mjini Dakar na sehemu zengine REUTERS - ZOHRA BENSEMRA
Matangazo ya kibiashara

Maandamano bado yanashuhudiwa katika mji mkuu Dakar, na Ziguinchor, eneo ambako kiongozi wa upinzani Ousmane Sonko ni meya.

Hatua ya kukamatwa kwa Sonko na kufutwa kwa chama chake cha kisiasa wikendi iliyopita imeaamsha maandamano mapya.

Sonko ambaye anazuiliwa na polisi, ametangaza kuaanza mgomo wa kususia chakula akiwa gerezani.

Kiongozi wa upinzani nchini  Senegal Ousman Sonko amesema ameanza mgomo wa kususia chakula gerezani
Kiongozi wa upinzani nchini Senegal Ousman Sonko amesema ameanza mgomo wa kususia chakula gerezani REUTERS - COOPER INVEEN

Siku ya Jumatatu waziri wa mambo ya ndani nchini humo Antoine Félix Abdoulaye Diome, alitangaza kwamba serikali imefuta chama cha (Pastef) chake Sonko kwa tuhuma za kuchochea vurugu zilizoshuhudiwa jijini Dakar mwezi uliopita.

Video kwenye mitandao ya kijamii zimeonyesha waandamanaji wakiwarusha maofisa wa usalama mawe kufutia hatua hiyo ya kukatwa kwa kiongozi wao na kuvunjwa kwa chama chake.

Wafuasi wa upinzani wamekuwa wakiituhumu serikali kwa kumvuruga kiongozi wao
Wafuasi wa upinzani wamekuwa wakiituhumu serikali kwa kumvuruga kiongozi wao © Leo Correa / AP

Hii ni mara ya tatu chama cha kisiasa kinavunjwa katika taifa hilo la Afrika Magharibi tangu kujipatia uhuru wake kutoka kwa Ufaransa mwaka wa 1960.

Wafuasi wa Pastef wamemtuhumu rais wa Macky Sall na chama chake tawala kwa kujaribu kumfungia nje mpinzani wake ambaye pia aliibuka wa tatu katika uchaguzi wa urais wa 2019.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.