Pata taarifa kuu

Mali yakashifu hatua ya Marekani kutangaza vikwazo dhidi ya maofisa wake

Waziri mkuu wa Mali Choguel Kokalla Maïga, amekashifu hatua ya Marekani kutangaza vikwazo kwa waziri wa ulinzi nchini humo, mkuu wa jeshi la angani na naibu wake, kiongozi huyo akisistiza kuendelea kuunga mkono utawala wa kijeshi.

Waziri mkuu wa Mali, Choguel Maïga amesema wataendelea kuunga mkono maofisa wa kijeshi nchini humo
Waziri mkuu wa Mali, Choguel Maïga amesema wataendelea kuunga mkono maofisa wa kijeshi nchini humo AFP - FLORENT VERGNES
Matangazo ya kibiashara

Choguel amesema kuwa vikwazo dhidi ya waziri wa ulinzi Kanali Sadio Camara, Jenerali Alou Boi Diarra, Kanali Adama Bagayoko, havina malengo yoyote isipokuwa kuvuruga watu wa Mali.

Aidha kiongozi huyo ameeleza kwamba hakuna kitakachotuvuruga watu wa taifa hilo kutoka kwa malengo yake kujenga upya Mali.

Wizara ya fedha ya Marekani, ilitangaza vikwazo kwa watatu hao kwa kwa tuhuma za "kuwezesha" upanuzi wa kundi la Wagner la Urusi nchini Mali.

Wanajeshi wa Wagner wametuhumiwa kwa kufanya ukatili pamoja na jeshi la Mali katika vita vyao dhidi ya wanajihadi, huku Marekani ikisema kuwa vifo vya raia vimeongezeka zaidi ya mara tatu tangu mamluki hao walipotumwa nchini humo mwishoni mwa 2021.

Waziri mkuu ndiye afisa mkuu pekee katika serikali ya kijeshi aliyetoa maoni yake kuhusu vikwazo hivyo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.