AU yatetea uamuzi wake wa kuwafukuza wawakilishi wa Israel
NAIROBI – Umoja wa Afrika umetetea uamuzi wake wa kuwafukuza wawakilishi wa Israel katika kikao cha wakuu wa nchi kilichofanyika mwishoni mwa juma lililopita, AU ikisema hadhi ya Israel kama mualikwa kwenye umoja huo ilisitishwa kwa muda.
Imechapishwa:
Cheza - 00:23
Maelezo ya AU yamekuja baada ya balozi wa Israel, Sharon Bar-li kuondolewa kwa nguvu kwenye mkutano huo.
Musa Faki Mahamat, ni mkuu wa kamisheni ya umoja wa Afrika.
“Hatukuwa tumetoa mwaliko wowote kwa afisa yeyote wa Israel kuhudhuria mkutano huu.”ameeleza Musa Mahamat
Kikao cha wakuu nchi kilichofanyika Jumapili iliyopita, kilijadili changamoto za bara la Afrika ikiwemo mapinduzi ya kijeshi, mizozo na mabadiliko ya tabia nchi.