Kenya: Maofisa wa polisi wanaswa wakijaribu kuwaibia raia
Kituo kimoja cha televisheni nchini Kenya kimesambaza picha za video zikiwaonyesha maofisa wanne wa polisi wanaodaiwa kujaribu kuwaibia watu wawili shilingi za Kenya milioni 2 ($16,000; £13,000) kwenye barabara moja jijini Nairobi.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Waathirika waweroptiwa kuwa wafanyikazi katika duka la kubadilisha pesa ambapo walikuwa wametoa pesa kutoka benki iliyokuwa karibu.
Jaribio hilo la wizi liliripotiwa kuzimwa baada ya tahadhari kutolewa.
Polisi Waliopanga Wizi:
— NTV Kenya (@ntvkenya) January 10, 2023
Maafisa wanne wafikishwa mahakamani baada ya kujaribu kumuibia mfanyabiashara mmoja kwenye ofisi ya kubadilisha fedha za Forex takriban millioni mbili nukta tano#NTVJioni @NginaKirori pic.twitter.com/CygfwPQXv7
Maofisa hao wa Polisi walikamatwa baadaye baada ya wenzao kulinasa gari walilokuwa wakitumia kufanya uhalifu huo.
Wamefikishwa katika mahakama moja jijini Nairobi kwa makosa ya kujaribu kuwaibia raia.