UGANDA-SIASA
Uganda: Mahakama yaagiza kufutwa kwa kipengele tata cha sheria
Nchini Uganda, Mahakama ya Katiba jijini Kampala, imeagiza kufutwa kwa kipengele tata cha sheria cha mawasiliano na matumizi mabaya ya Kompyuta, kilichokuwa kinatumiwa kuwabana wanasiasa wa upinzani, wanahabari na wanaharakati, wanaoikosoa serikali. Mahakama imesema sheria hiyo ni kinyume cha Katiba, inayoeleza haki ya kujieleza nchini humo. Kutoka Kampala, Mwandishi wetu Kenneth Lukwago anaeleza zaidi..........
Imechapishwa:
Cheza - 01:30