Pata taarifa kuu
DRC

Waasi wawaua watu 22 Wilayani Beni Mashariki mwa DRC

Nchini DRC, watu 22 wameuawa  katika kijiji cha Beu Manyama Kilomita 40 Kaskazini Magharibi mwa Beni.

Hasara iliyojitokeza katika eneo lililoshambuliwa na waasi wa ADF
Hasara iliyojitokeza katika eneo lililoshambuliwa na waasi wa ADF RFI/Patient Ligodi
Matangazo ya kibiashara

Maafisa wa usalama, wanadai waasi wa ADF ndio waliohusika na mauaji hayo.

Kanali Charles Omeonga, ni kiongozi wa kijeshi katika Wilaya ya Beni amesema kinachofanywa na jeshi kuwalinda raia.

Mauaji yalitokea katika eneo la Beu, waasi walijificha katika eneo hilo, jeshi linaendelea kufukuzana na waasi kila wakati.

Kuendelea kwa mauaji ya raia yameendelea kushuhidiwa Wilaya Beni, licha ya kuwepo kwa uongozi wa jeshi na wanajeshi wa Uganda wanaopambana na waasi wa ADF.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.