Pata taarifa kuu
DRC-USALAMA

Waasi wa ADF waihama ngome yao kufuatia mashambulizi ya kijeshi ya Uganda na DRC

Waasi wa ADF ambao wameshtumiwa kuendeleza maafa ya maelfu ya raia Mashariki mwa DRC kwa sasa wanahamia maeneo ya Magharibi kutoka kwenye ngome yao, karibu na mpaka wa Uganda.

Askari wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (FARDC) wakipiga doria katika kijiji cha Kaswara, kilomita 60 kusini magharibi mwa Bunia, katika mkoa wa Ituri mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Julai 14, 2006.
Askari wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (FARDC) wakipiga doria katika kijiji cha Kaswara, kilomita 60 kusini magharibi mwa Bunia, katika mkoa wa Ituri mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Julai 14, 2006. REUTERS
Matangazo ya kibiashara

Hatua hii inaelezwa na wachambuzi wa masuala ya vita, kufuatia operesheni za kijeshi zinazoongozwa na Uganda tangu mwishoni mwa mwezi Novemba mwaka 2021.

Kwa kipindi cha wiki moja pekee, katika Wilaya ya Beni huko Kivu Kaskazini na Irumu, mkoani Ituri, raia 79 wameuawa baada ya waasi hao kuvamia vijiji sita.

Tangu mwaka 2019, Wilaya ya Irumu ndio iliyoathiriwa zaidi, tangu kundi hilo lianze mashambulizi dhidi ya raia, lakini Beni pia imekuwa ikishambuliwa tangu mwaka 2014.

Mbunge kutoka Goma Jean-Baptiste Muhindo Kasekwa, anasema kati ya Machi 9 mpaka 14, watu 96 wameuawa Wilayani Beni na Irumu, wengine 383 tangu operesheni za jeshi la Uganda na zaidi ya Elfu mbili tangu kuanza kutekelezwa kwa hali ya dharura katika maeneo hayo mwezi Mei mwaka uliopita.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.