Pata taarifa kuu
AFRIKA KUSINI-RUSHWA-UCHUMI

Mtoto wa rais wa Afrika Kusini akiri kupokea hongo

Mtoto wa rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa, Andile, amekiri kwamba alipewa kitita cha dola za Marekani Laki moja na elfu arobaini kutoka kwa kampuni inayokabiliwa na mashtaka ya rushwa.

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa, ambaye mtotot wake amekiri kupewa hongo wakati wa utawala wa Jacob Zuma.
Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa, ambaye mtotot wake amekiri kupewa hongo wakati wa utawala wa Jacob Zuma. © AFP
Matangazo ya kibiashara

Wadadisi wanasema tukio hilo linaweza kumvuruga baba yake kuelekea kwenye uchaguzi mkuu mwezi Mei mwaka huu.

Ramaphosa kwa sasa anakabiliwa na kibarua kigumu cha kukisafisha chama cha ANC kuhusu madai ya ufisadi kuelekea uchaguzi Mkuu tarehe nane mwezi Mei.

Kampuni ya Bosasa ambayo kwa sasa inaitwa African Global Operations inadaiwa kutowa masoko hewa ya zabuni na kusaini mikataba na serikali ambapo takriban dola milioni 120 zilipotea.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.