Viongozi wa mataifa ya Afrika mashariki wanakutana leo mjini Daresalaam kujadili mzozo wa Burundi
Imechapishwa:
Cheza - 16:50
Katika mjadala wa wiki, hii leo tunaangazia mkutano wa viongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambao unafanyika hii leo hapa jijini Dar es salaam nchini Tanzania kujadili hali ya kisiasa katika taifa la Burundi.Nchini Burundi kwenyewe maandamano yameendelea kushuhudiwa jijini Bujumbura na leo , mwandamanaji mmoja ameuawa baada ya kupigwa risasi na polisi wakati alipokuwa ameungana na wenzake katika maandamano hayo ya kumshinikiza rais Piere Nkurunziza kutowania urais kwa muhula wa tatu.Kulizungumzia hili tumewaalika Abdulkarim Atiki ni mchambuzi wa masuala ya siasa Dar es salaam Tanzania, naye Alhaji Mali Ally, mchambuzi wetu wa masuala ya siasa akiwa Mjini Bujumbura nchini Bujumbura,Ungana na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka kusikiliza,.............