Usalama kuimarishwa nchini Kenya baada ya mauaji ya Mandera
Imechapishwa:
Cheza - 11:13
Katika Makala mjadala wa wiki hii leo, tunazungumzia hali ya Usalama nchini Kenya ambako mwishoni mwa juma lililopita kundi la Al Shabaab liliwauwa kwa kuwapiga risasi zaidi ya watu 28 waliokuwa wakisafiri kwenye basi moja karibu na mpaka wa Somalia.Maafisa wa ngazi ya juu wamesema kuwa basi hilo lilitekwa nyara katika Jimbo la Mandera wakati likiwa njiani kuelekea jijini Nairobi.Kulizungumzia hili nimewaalika kwenye laini ya Simu Mwenda Mbijiwe ni mtaalamu wa masuala ya kiusalama, akiwa nairobi Nchini Kenya,lakini pia Brian wanyama akiwa Bungoma nchini Kenya.Karibu kuungana na mwandishi wetu Reuben Lukumbuka.