Pata taarifa kuu

Burundi: Tume ya uchaguzi yaendelea kunyooshea kidole

Wajumbe wa tume ya uchaguzi kwenye ngazi za wilaya nchini Burundi wanatazamiwa kula kiapo Jumatano Novemba 5, huku chama cha NFL kikisema bado hakijapata jibu kuhusu kasoro zilizoibuka kuhusu uteuzi wa wajumbe hao, kwa maandalizi ya Uchaguzi wa mwaka wa 2016.

Tume ya uchaguzi nchini Burundi ilinyooshewa kidole cha lawama kwa jinsi ilivyoandaa chaguzi za mwa ka 2010, na kwa sasa bado  inaendelea kunyooshewa kidole.
Tume ya uchaguzi nchini Burundi ilinyooshewa kidole cha lawama kwa jinsi ilivyoandaa chaguzi za mwa ka 2010, na kwa sasa bado inaendelea kunyooshewa kidole. AFP / Esdras Ndikumana
Matangazo ya kibiashara

Muungano wa vyama vya upinzani ADC-Ikibri pamoja na baadhi ya mashirika ya kiraia viliamua hivi karibuni kuwaondoa wajumbe wao katika tume hiyo.

Tume huru ya kitaifa ya uchaguzi nchini Burundi Ceni, imekua ikinyooshewa kidole na vyama vya upinzani, mashirika ya kiraia pamoja na vyama vinavyounga mkono utawala wa chama tawala Cndd-fdd kwa kuchukua uamzi bila kuwashirikisha wadau wote katika suala la uchaguzi.

Tume hiyo ilipingwa na vyama vya upinzani tangu ilipoteuliwa na kupasishwa na Bunge mwanzoni mwa mwaka 2014. Hata hivo tume hiyo Ceni ilituhumiwa katika uchaguzi wa mwaka 2010 kwamba ilipanga njama na chama tawala Cndd-Fdd kwa kuiba kura, ziliyopelekea ushindi wa chama cha Cndd-Fdd.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.