Kundi la Al Shabab laonya kuendeleza mashambulizi Somalia
Kundi la wanamgambo wa Al-Shabab nchini Somalia limekiri kuhusika na mfululizo wa mashambilizi ya mabomu kwenye mji mkuu Mogadishu na kuonya kuwa litaendelea na mashambulizi haya hata wakati huu wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Imechapishwa:
Cheza - 03:06
Msemaji wa kundi hilo, Abdulaziz Abu Musab amethibitisha wapiganaji wake kutekeleza mashambulizi matano ya mabomu Jumatatu ya wiki huu kwenue mji wa Mogadishu na kuapa kuzidisha mashambulizi yao wakati huu wa mfungo.
Licha ya usalama kuimarishwa kati ya vikosi vya Serikali na vile vya kulinda amani ncini humo AMISOM, wachambuzi wa masala ya usalama wanaona hali bado ni tete nchini Somalia na usalama inabidi kudhibitiwa kama anavyoeleza hapa Mwenda Mbijiwe akiwa jijini Nairobi nchini Kenya.