Pata taarifa kuu
Sudan-upinzani

Mpinzani mwingine akamatwa nchini Sudan

Polisi nchini Sudan jana imemkamata kiongozi mwingine wa upinzani nchini humo Ibrahim al-Sheikh wakimtuhumu kutoa hotuba ya kichochezi wakati alipofanya mkutano wa hadhara magharibi mwa jimbo la Kordofan.

rais wa Sudani, Omas Hassan Al Bashir
rais wa Sudani, Omas Hassan Al Bashir
Matangazo ya kibiashara

Ibrahim al-Sheikh ambaye ni kiongozi wa chama cha Sudanese Congress alikamatwa akiwa nyumbani kwake na maofisa wa Polisi ambao walidai wanamshikilia kwa mahojiano kutokana na matamshi yake aliyoyatoa wakati wa mkutano wa kisiasa.

Kiongozi huyo wa upinzani aliyekamatwa mjini Nouhoud kitongoji kilichokopo Kordofan magharibi, huenda akakatiwa adhabu ya kifo iwapo atakutikana na makosa

Kukamatwa kwa Ibrahim al-Sheikh kunakuja ikiwa yamepita majuma kadhaa toka kiongozi mwingine wa kisasa na aliyewahi kuwa waziri mkuu wa taifa hilo, Sadiq al-Mahdi kukamtwa na polisi kwa tuhuma za uchochezi kwenye jimbo la kordofan.

Wanasiasa nchini humo wanaona kuwa huu ni mpango wa Serikali ya rais Omar al-Bashir kutaka kudhoofisha upinzani na kwamba hata viongozi hao wakiachiwa hali haitabadilika.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.