Pata taarifa kuu
KENYA

Polisi watano na raia wawili wauawa katika shambulizi mpakani mwa Kenya na Somalia

Polisi watano na raia wawili wameuawa katika shambulizi dhidi yao lililofanywa na watu waliojihami kwa silaha kwenye mpaka wa Kenya na Somalia,jeshi la polisi nchini kenya limethibitisha. 

Kambi ya Daadab mpakani mwa Kenya na Somalia
Kambi ya Daadab mpakani mwa Kenya na Somalia unhcr.org
Matangazo ya kibiashara

Shambulizi hilo limefanyika katika barabara iliyoko kati ya kambi kubwa zaidi ya wakimbizi duniani ya Dadaab na mji wa Mashariki wa Liboi wakati askari hao walipokuwa wakishika doria .

Taarifa zaidi kutoka nchini Kenya zinaeleza kuwa polisi wengine wawili bado hawajulikani walipo kufuatia tukio hilo.

Mpaka wa Kenya na Somalia umekuwa kitovu cha mashambulizi ya kuvizia yanayofanywa na watu wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa Al Shabaab pamoja na makundi mengine ya watu waliojihami.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.