Raia mmoja wa Kenya afunguliw amashtaka na mahakama kwa kosa la la mauaji
Mahakama moja nchini Kenya imemfungulia mashtaka ya mauaji na utekaji nyara raia wa nchi hiyo Ali Babitu Kololo kwa tuhuma za kupanga mauaji ya raia wa Uingereza David Tebbuti na utekaji nyara wa mkewe Judith wakati wakiwa kwenye hoteli moja ya kitalii mjini Lamu.
Imechapishwa:
Mwendesha mashtaka katika kesi hiyo amesema kuwa Kololo anashtakiwa kwa kuhusishwa kuwa na mahusiano na kikundi cha watu ambao walihusika na mauaji hayo pamoja na utekaji nyara wa rais huyo wa Uingereza.
Wakili anayemtetea Kololo, George Wakohiu amesema kuwa anaamini mteja wake hana hatia na kuwa mahakama hiyo itampatia dhamana.
Maofisa usalama nchini kenya wanasema kuwa huenda watekaji nyara hao wakawa wanamshikilia mateka Judith wakiwa nchini Somalia.