Viongozi wakuu nchini Tanzania wadiriki kisomo maalum kwa waliokufa katika ajali ya meli
Viongozi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, wamekutana visiwani Zanzibar kuungana na waathiriwa na manusura kuwaliwaza, wa ajali ya meli iliyotokea mwishoni mwa juma na kusabisha mauji ya watu 197 katika bahari ya hindi.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Cheza - 00:52
Kulingana na taarifa rasmi ya serikali ya Tanzania watu 197 waliuawa huku 619 wakiokolewa wakiwa hai. Hata hivyo kumekuwa na taarifa kwamba huenda miili ya watu wengine waliokuwemo katika meli hiyo haijapatikana.
Serikali ya Afrika Kusini, imewatuma wataalamu wake kusaidizana na watanzania katika shughuli za kutafuta miili na mabaki ya meli hiyo.
Kisomo maalum kwa waliokufa na waliojeruhiwa katika ajali hiyo ya MV Spice irlanders kimefanyika huko Zanzibar.